Na Rahma Khamis na Mwanaisha Moh’d Maelezo-Zanzibar.
Mkutano wa Kumi na Tisa (19) wa
Baraza la Nane (8) la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza siku ya
Jumatano Tarehe 11 March, 2015 saa 3:00 kamili za asubuhi ambapo miswada
minne ya sheria itawasilishwa na kujadiliwa barazani hapo.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Baraza
la Wawakilishi Nd. Yahya Khamis Hamad alipokuwa akizungumza na
Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Baraza hilo huko Chukwani nje
kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Amesema miswada itakayojadiliwa ni
pamoja na Mswada wa Sheria ya kufuata Sheria ya Miradi ya Maridhiano
Namba 1 ya mwaka 1999, Kutunga Sheria kwa ajili ya kuazishwa na
kuendesha mashirikiano baina ya Sekta za Umma na Sekta Binafsi zilizopo
nchini ikiwemo na Kuwasilishwa mbele ya Baraza, Sheria ya Kura ya Maoni
No. 11 ya Mwaka 2013 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa
kifungu 132(2) cha Katiba ya Zanzibar.
Vile vile Katibu huyo
ametanahabahisha kuwa mswada mwengine utakaojadiliwa ni pamoja na
kuanzishwa kwa Baraza la Sensa ya Filamu na Utamduni Zanzibar ambalo
litasaidia kukuza na kulinda utamaduni wa Wazanzibari.
Sambamba na hayo amesema katika
shughuli zitakazoendelea katika Baraza hilo ni pamoja na maswali na
majibu ambayo yataulizwa na kujibiwa na wajumbe wa baraza hilo ambapo
maswali 77 yanatarajiwa kujibiwa katika baraza hilo.
Katibu Yahya amewaomba Wajumbe wa Baraza hilo kufika kwa wakati barazani hapo ili kwenda sambamba na muda kwa lengo la kutimiza majukumu yaliokusudiwa katika mkutano huo.
Wednesday, March 11, 2015
Mkutano wa 19 baraza la wawakilishi kuanza jumatano
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Blog Archive
-
▼
2015
(23)
-
▼
March
(7)
- MAMA MARIA NYERERE AKANUSHA UVUMI ULIOENEA JANA KU...
- MAHAKAMA KUU YAFUTILIA MBALI KESI ILIYOFUNGULIWA N...
- Balozi wa China akutana na Rais Dk.Shein
- Mkutano wa 19 baraza la wawakilishi kuanza jumatano
- Serikali kuendelea kuandaa mazingira bora ya wavuv...
- Serikali yajidhatiti Kudhibiti Makosa ya Utakatish...
- ZINDUKA Vocational Training Center Students:
-
▼
March
(7)
No comments:
Post a Comment