N.I.H.F -KIKOA

N.I.H.F -KIKOA
N.I.H.F -KIKOA

FOREPLAN CLINIC

FOREPLAN CLINIC
FOREPLAN CLINIC

Thursday, August 14, 2014

Students earn millions by investing in bourse

Dar es Salaam Stock Exchange chief executive officer Moremi Marwa speaks in a past event. PHOTO | FILE      
By Alawi Masare The Citizen Reporter

Posted  Thursday, August 14  2014 at  12:20
In Summary
University students who participated in the DSE scholar investment challenge 2014 that ran between April and July each created wealth of that amount.
Dar es Salaam. It is possible for one to create wealth of Sh4.1 million in three months with capital of Sh1 million at the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE).
That can be done by buying and selling shares at the bourse.
University students who participated in the DSE scholar investment challenge 2014 that ran between April and July each created wealth of that amount.
That means the buying of shares may have good returns, according to stock market experts who attended the award conferring ceremony yesterday.
The first winner of the challenge, Mr Laurent Dyanko, a first-year horticulture student at the Morogoro-based Sokoine University of Agriculture created wealth of Sh4.1 million in the three months by buying and selling shares of different counters at the bourse.
If the Sh1 million was saved in a fixed account with the commercial banks which offer a maximum of 10 per cent interest per year, the owner of the money would have earned mere Sh1.1 million at the end of the year.
“I worked on advice given by economic experts and also used the DSE online information to understand the trend in share prices. I’m sure anyone can gain even more than this with just a little capital,” said Mr Dyanko.
Shares of companies like Tanzania Breweries Limited (TBL) and NMB Bank listed at the DSE rallied by 65.43 per cent and 56.49 per cent between January 1 and August 12 this year respectively, according to Tanzania Securities Tuesday report.
DSE, Financial Sector Deepening Trust and NMB launched the challenge to the higher learning institutions as part of efforts to encourage locals to participate in the stock market.
Currently, only about 200,000 Tanzanians participate in the bourse due to low awareness and the fact that the concept is still new, according to DSE chief executive officer Moremi Marwa. DSE was launched in 1998.
“There is stereotype that only rich people can invest in capital markets. This is not true,” said Mr Marwa.
About 5,000 students participated in the competition but only top 50 were awarded certificates

Nacte Inter College TANZANIA Debate Competition

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133.

Mratibu wa Tamasha la Vyuo vya Elimu ya Kati Tanzania( NACTE INTER COLLEGE TANZANIA 2014-2015, Bi, Magreth Kilawe,(kulia) akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari. kuhusiana na Michezo hiyo katika Vyuo vya NACTE TANZANIA

Mashindano ya Mijadala kwa kwa vyuo vya Elimu ya Kati kwa kanda ya Dar es Salaam, yanatarajiwa kuanza Novenber mwaka huu.
Akizungumzia katika semina elekezi, iliyowakutanisha baadhi ya walimu wa mijadala kutoka katika  Vyuo mbalimbali, Mratibu wa Tamasha la Nacte Inter College Tanzania 2014/2015, Magreth Kilawe, kutoka Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania, ambao ndio waandaji wa Tamasha hilo, Bi Magreth Milawe, amesema jumla ya Vyuo 33 kutoka Kanda ya Dar es Salaam,Vimeshathibitisha ushiriki wao katika Tamasha hilo ambalo ni la kwanza kufanyika Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Mratibu wa Tamasha la NACTE INTER COLLEGE TANZANIA 2014/2015

: Bi, Magreth Kilawe


Bi, Magreth, amesema Tamasha hilo pia litaonyeshwa kwenye moja ya runinga hapa nchini kuwapa fursa watazamaji kushuhudia vipaji vya wanafunzi katika kujieleza mbele ya jamii.
Amesema nia na madhumuni ya Tamasha hilo, mbali na kuondoka na kitita cha zawadi kwa washindi lakini pia ni njia mojawapo ya kuinua kiwango cha elimu hapa nchini kwa wanafunzi kupata nafasi ya kujieleza mbele za watu, kufanya utafiti kutokana na mada itakayowekwa mezani, kuweka mahusiano mema dhidi ya wanafunzi na kujenga kizazi kipya katika nyanja ya elimu kupitia mfumo wa mijadala.

Bi, Magreth Kilawe(kulia) kushoto ni Mwakilishi wa Viongozi Serikali ya Wanafunzi Mr.Stephano

Vyuo vilivyojitokeza mpaka sasa miongoni mwa vyuo 105 kushiriki Tamasha hilo mpaka sasa ni
26.Lugalo Military Medical School - Dar es Salaam 
32. Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) - DSM
Kwa Mujibu wa Bi, Magreth,nafasi za ushiriki bado zipo kwa vyuo ambavyo bado havijathibitisha ushiriki na kwamba mwisho wa Usajili ni tarehe moja mwezi wa tisa mwaka huu.
Maandalizi yanaendelea vizuri mpaka sasa tunaendelea na mazungumzo na wadhamini na ambao tayari wameonyesha nia ya kusaidia Michezo hii ya NACTE katika vyuo vya Elimu ya Kati ni Pamoja na N.M.B, P.S.P.F, TCRA,AZAM, CXC TOURS,PCCB,LAPF,TAHA, BANK YA POSTA,MALT MEDIA GROUP, NSSF,TTCL,FAST-JET,IKONDOLELO LODGE, Global Publishers, East Afrika Radio Radio & TV,Clouds Media Group"pamoja na mtandao wa www.shaabanmpalule.blogspot.com(FULL UTAMU-JUMWAGE), ameongeza Bi, Magreth
Michezo mingine katika tamasha hilo ni pamoja na Soka, Netball,Basketball,Handball, Voleyball, Marathoni,Vipaji vya Utangazaji,Mashindano ya DJ's, Shindano la Mavazi ya Ofisini,Uongozi na Utawala, pamoja na Vipaji vya Kuimba (Muziki).
Fulsa hiyo ya uwepo wa michezo kwenye vyuo vya elimu ya kati Tanzania, imekuja baada ya hitaji la muda mrefu kutoka kwa wanafunzi waliokuwa wakitoka kwenye Shule za Sekondari kujiunga katika Vyuo vya Elimu ya Kati, ambapo walikuwa hawapati fulsa ya kukutana kimichezo katika kubadilishana mawazo na kutengeneza mahusiano mema miongoni mwa Wanafunzi, Walimu na Wadhamini.
Hata hivyo Bi, Magreth amesisitiza kwamba, wakati wa Tamasha Msisimko mkubwa utakuwa kwa washiriki wa Mijadala(Debate Competition)na kwamba baada ya kukamilika tamasha la Kanda ya Dar es Salaam, itafuata Kanda ya Mikoa ya Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma na Zanzibar,katika kipindi cha 2014/ 2015.
Michezo yote itachezwa kwenye viwanja vilivyopendekezwana Kamati Kuu ya NACTE INTER COLLEGE TANZANIA, mbavyo ni
The Mwalimu Nyerere Memorial Academy, University of Dar es Salaam, TCC Chang’ombe, Kibaha Secondary, Gymkhana Posta, na Leaders Club.

ZANZIBAR YAIKARIBISHA UJERUMANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133.
Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke na Rais SheinSERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeiomba Serikali ya Ujerumani kupanua uwekezaji katika nyanja za viwanda vidogo vidogo pamoja na bahari kuu ili kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.
Makamu wa kwanza wa Rais wa  Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad  alitoa ombi hilo alipokutana kwa mazungumzao na Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke  aliyefika kwa ajili ya kujitambulisha.
Maalim Seif alisema miongoni mwa matatizo makubwa yanyoikabili Zanzibar kama nchi nyingine za Afrika ni vijana wengi kukosa ajira na shughuli za kujiletea maendeleo, hivyo Ujerumani inayo nafasi kubwa ya kupambana na jambo hilo.
Hata hivyo, alisema miongoni mwa njia muafaka ya kuweza kufanikisha azma hiyo, ni nchi hiyo kuelekeza nguvu zaidi katika kusaidia elimu ya amali ambayo itawawezesha vijana wa Zanzibar wakiwemo wale wanomaliza masomo kuweza kupata mbinu za ajira.
Aliongeza kuwa Zanzibar imeweza kupiga hatua kubwa katika sekta ya elimu lakini bado inayotolewa haijakuwa na ubora unaowezesha vijana kukabiliana na changamoto za uhaba wa ajira.
Seif alisema fursa nyingine muhimu za ushirikiano kati ya nchi mbili hizo ni katika sekta ya utalii na kilimo.
Naye Balozi Konchanke alisema amepokea maombi hayo na yatazingatiwa katika mipango ya ushirikiano wa nchi yake na Tanzania.
Alisema anaelewa kuwa Zanzibar inazo fursa muhimu za kiuchumi na biashara, ikiwemo kilimo cha viungo na utalii ambazo wawekezaji wa Ujerumani wanaweza kuzitumia katika kufungua miradi yao.
Alisema kuwa atakuwa balozi katika kuiuza Tanzania na Zanzibar kwa wawekezaji wa Ujerumani kwani wanaweza kuzitumia kwa kufungua miradi yao.
Chanzo:Tanzania Daima

NAIBU WAZIRI MASELE AWATAKA VIJANA KUJIKITA KATIKA MAMBO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

 Rais wa Vijana Wanasayansi Duniani Bw. Meng Wang (kulia) akimkabidhi kinyago cha tembo Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Rais wa Vijana Wanasayansi Duniani Bw. Meng Wang (kulia) akimkabidhi zawadi ya Kipepeo Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele (aliyesimama kulia) akimkabidhi ramani ya Afrika iliyochongwa kwa mti Rais wa Wajiolojia Afrika Profesa Aberra Mogessie wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

 Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele (kulia) akimkabidhi zawadi Kijana Mwanasayansi Duniani toka nchini India wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele (kushoto) akimkabidhi zawadi Kijana Mwanasayansi Duniani toka nchini Botswana wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Vijana Wanasayansi Duniani wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere. Wa kwanza kulia ni Makamu Mwenyekiti na Mwakilishi wa Vijana Wanasayansi Duniani (YES) na anaemfuatia ni Rais wa YES Bw. Meng Wang. Wa kwanza toka kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Tanzania, Profesa Abdulkarim Mruma akifuatiwa na Rais wa Wajiolojia Afrika Profesa Aberra Mogessie.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.



 Rais wa Vijana Wanasayansi Duniani Bw. Meng Wang akitoa maelezo machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Tanzania, Profesa Abdulkarim Mruma akitoa nasaha zake mbele ya Vijana Wanasayansi Duniani (hawapo pichani) wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele akiwahutubia Vijana Wanasayansi Duniani wakati alipokuwa akifunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Meza Kuu ambapo katikati ni Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Stephen Masele, kulia ni Rais wa Vijana Wanasayansi Duniania Bw. Meng Wang na kushoto ni Rais wa Wajiolojia Afrika Profesa Aberra Mogessie.
 Baadhi ya Vijana Wanasayansi Duniani waliohudhuria siku ya ufungaji Kongamano wakifuatilia kwa makini hotuba ikiyotolewa na mgeni rasmi wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.





 Rais wa Vijana Wanasayansi Duniani (YES), Bi. Elyvin Nkhonjera kutoka nchini Malawi akikaribisha wageni waalikwa wakati wa kufunga Kongamano la Tatu la Wanasayansi Vijana Duniani lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
NAIBU WAZIRI MASELE AWATAKA VIJANA KUJIKITA KATIKA MAMBO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
14/08/2014.
NAIBU Waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele amewataka vijana nchini kupenda kujikita katika masomo ya sayansi na teknolojia kama mihimili yenye kuleta maendeleo kwa haraka ulimwenguni ili waweze kupata ujuzi na mitazamo katika sekta ya gesi ambayo inakuwa kwa kasi kubwa nchini.
Mhe. Masele ameyasema hayo jana wakati alipokuwa akifunga Kongamano la Tatu la Vijana Wanasayansi Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere, kongamano ambalo liliwakutanisha vijana toka nchi zaidi ya 46 ulimwenguni zikiwemo baadhi ya nchi za Afrika ambapo Tanzania ilikuwa mwenyeji wa Kongamano hilo.
Mhe. Masele ameeleza kuwa sayansi na teknolojia ndiyo mihimili mikubwa ya sasa katika kuleta maendeleo ya haraka katika nyanja mbalimbali kwani mambo mengi hivi sasa hutegemea sayansi na teknolojia.
Aidha, Mhe. Masele amezitaja baadhi ya changamoto zinazozikabili baadhi ya nchi za Afrika katika kupata maendeleo ni pamoja na kutowekeza katika sayansi na teknolojia hali inayopelekea baadhi ya nchi nyingi kukosa wataalam wa kutosha katika mambo ya sayansi na teknolojia, hivyo amezitaka nchi za Afrika kuwekeza katika sayansi ili kuweza ili kubadilisha uchumi wa Afrika.
“Sayansi na teknolojia huleta maendeleo makubwa hivyo nawapa moyo vijana muendelee kufanya kazi kwa bidii na kujituma katika mambo ya sayansi na teknolojia ili muweze kuleta uchumui endelevu”. Alisema Masele.
Akizungumzia kwa upande wa Serikali ya Tanzania, Mhe. Masele amesema kuwa serikali ya Tanzania imewekeza nguvu zake kwa sasa katika kuendeleza sayansi ya afya kwa kuanzisha Vyuo mbalimbali na kuwasomesha watanzania nchi mbalimbali za nje ili waweze kwenda kupata ujuzi na kuwa wataalam na wakaguzi katika sekta ya gesi pamoja na mafuta kwa lengo la kuja kuisaidia nchi yao.
“Wajibu wetu kama Serikali tumeamua kwa makusudi kusomesha vijana katika nchi mbalimbali ili wakaweze kupata elimu juu ya sayansi na teknolojia hasa katika masuala ya gesi ili kupata wataalam na wakaguzi wa kutosha nchini ambao watalisaidia taifa kuinua uchumi wake na hivi sasa serikali imeanzisha vyuo mbalimbali nchini, program mbalimbali za mafunzo kwa watanzania, imetoa ufadhili wa masomo kwa watanzania na imedhamini makongamano ya vijana ili wapate fursa ya kujiendeleza.” Alisisitiza Masele.
Mhe. Masele amempongeza Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo kwa kazi kubwa anayoifanya katika Wizara yake na pia amewapongeza vijana waliohudhuria katika kongamano hilo pamoja kuyapongeza Makampuni wadhamini wa kongamano hilo na kuyataka makampuni hayo kuendelea kuwekeza pamoja na kulipa kodi ili serikali iweze kukusanya mapato na wananchi wapate kunufaika na mapato hayo.
Naye Rais wa Vijana Wanasayansi Duniani (YES) Bw. Meng Wang amemshukuru Makamu wa Rais wa Tanzania, Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Naibu Waziri steven Masele kwa kuwaunga mkono vijana waliohudhuria kongamano hilo na kuonesha hali nzuri ya ushirikiano baina ya serikali na vijana na amewaasa vijana kujikita katika sayansi na teknolojia kama mihimili mikuu ya maendeleo duniani.
“Naishukuru sana Tanzania pamoja na ujio wa Mawaziri wake katika kufanikisha kongamano hili la vijana wanasayansi, nawashukuru pia wadhamini wa makampuni mbalimbali wa kongamano hili pamoja na vijana kwa ujumla toka nchi mbalimbali duniani”. Alisema Wang.