N.I.H.F -KIKOA

N.I.H.F -KIKOA
N.I.H.F -KIKOA

FOREPLAN CLINIC

FOREPLAN CLINIC
FOREPLAN CLINIC

Sunday, September 21, 2014

UJUMBE WA CHAMA CHA FRELIMO CHA MSUMBIJI CHAKUTANA NA BAADHI YA WAJUMBE WA CHAMA CHA MAPINDUZI ZANZIBAR.

  Mjumbe wa Kamati ya CCM Taifa Bi. Khadija Hassan Aboud akimkaribisha Mbunge ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha FRELIMO cha Msumbiji Bi. Nyeleti Mondlane Ofisi kuu ya CCM Zanzibar.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha FRELIMO cha Msumbiji Bi. Nyeleti Mondlane akisaini kitabu cha wageni alipofika Ofisi kuu ya CCM Zanzibar (kulia) Katibu wa FRELIMO Zanzibar Bw. Agostino Andrea.
 Kiongozi wa Ujumbe wa Chama cha FRELIMO Bi. Nyeleti Mondlane (watatu kushoto) akibadilishana mawazo na wenyeji wake wajumbe wa Chama cha Mapinduzi katika Ofisi Kuu Kisiwandui Zanzibar ikiwa ni mkakati wa kuimarisha Uhusiano wa Vyama vyao na kuzindua Kampeni ya Uchaguzi Mkuu Nchini Msumbiji.
 Picha ya pamoja ya Ujumbe wa Chama cha FRELIMO na baadhi ya wajumbe wa Chama cha Mapinduzi CCM wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya CCM Taifa Bi. Khadija Hassan Aboud wakatikati.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.

=========  ========  ========
CHAMA cha FRELIMO kimesema Wananchi wa Msumbiji wataendelea kukumbuka na kuthamini juhudi mbali mbali zilizochukuliwa na Watanzania wakati wa harakati za ukombozi na kuwafanya kuwa watu huru.

Kauli hiyo imetolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha FRELIMO Bibi Nyeleti Mondlane, alipokuwa na mazungumzo maalum na Uongozi wa CCM Zanzibar, hapo Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui.

Amesema Wananchi wa Msumbiji wana kila sababu ya kuwapongeza Watanzania kutokana na misaada yao ya hali na mali, jambo lililosaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wa Msumbiji kujikomboa na kuishi wakiwa watu huru ndani ya nchi yao huru.

Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya FRELIMO na pia ni Mbunge, amesema nchi hiyo imo katika amani na utulivu mkubwa, hali inayotoa fursa kwa Serikali ya FRELIMO  kuweza kufanikisha shughuli za kimaendeleo kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Ametumia kikao hicho kutoa wito kwa Wana FRELIMO wanaoishi Zanzibar kuendeleza mashirikiano ya karibu na wananchi wa Tanzania, CCM na Serikali zake, ili umoja na maendeleo kwa wananchi wa pande zote mbili.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM Mhe. Khadija Hassan Aboud, amemuhakikishia Bibi Mondlane kuwa Chama Cha Mapinduzi kitafanya kila linalowezekana kuhakikisha uhusiano wa kihistoria baina ya CCM na FRELIKO unaendelezwa kwa nguvu zote.

Amesema Vyama vya CCM mrithi wa ASP na FRELIMO, vina undugu wa kihistoria uliodumu kwa miaka mingi na kumesisitiza haja kwa Viongozi wa Vyama hivyo wanapaswa kuuendeleza na kuudumisha kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizo.

Bibi Mondlane yupo Visiwani Zanzibar kwa ziara ya kikazi ya kichama, ambapo katika mazungumzo hayo aliongoza Ujumbe wa watu watano, akiwemo Balozi Mdogo wa Msumbiji nchini Zanzibar Bwana Jorge Augusto Menezes.

KINANA , NAPE WAITEKA KIBAHA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wakazi wa Kibaha mjini wakati wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano .
 Kikundi cha ngoma cha Kisamamwe kikitumbuiza ngoma ya Afrika kabla ya kuanza kwa mkutano wa hadhara ambapo Katibu Mkuu wa CCM alihutubia wananchi wa Kibaha mjini.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kibaha mjini ambapo aliwaambia wapinzani wamekosa hoja ya msingi kiasi cha kuamua kufanya maandamano ya kuleta vurugu nchini.
 Sehemu ya Umati wa watu wakisikiliza mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wana CCM wakiwa kwenye mkutano
 Mbunge wa Kibaha mjini Silvestry Francis Koka akihutubia wakazi wake na kuwaambia kuwa pamoja na jitihada zote anazofanya maji bado ni donda sugu ila ufumbuzi upo njiani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kibaha mjini wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaambia viongozi wa halmashauri hawana budi kukaa na wafanya biashara ndogo ndogo kujadili kodi kabla ya kuwapangia kuona kama wana uwezo wa kulipa ama hapana hii itasaidia kupunguza lawama na mikingamo baina ya wafanya biashara na halmashauri.

Friday, September 19, 2014

Tanzania, Thailand kushirikiana katika madini na vito

Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo (mwenye shati la batiki), akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Wafanyabiashara wa Madini ya Vito wa Thailand, walipotembelea Banda la Tanzania katika Maonesho ya 54 ya Vito na Usonara ya Bangkok, yaliyofanyika Septemba 9 hadi 13 mwaka huu.
Makamu wa kwanza wa Rais wa Taasisi ya Wafanyabiashara wa Madini ya Vito na Usonara wa Thailand, Bw. Sutipong Dumrongsakul, akimkabidhi zawadi maalumu Mkuu wa Ujumbe kutoka Tanzania ulioshiriki maonesho ya vito ya Bangkok, Archard Kalugendo, mara baada ya kikao kati ya Ujumbe huo na Viongozi wa Taasisi hiyo ya Wafanyabiashara wa Thailand.
Wateja mbalimbali wakihudumiwa katika Banda la Tanzania kwenye maonesho ya vito na usonara ya Bangkok yaliyofanyika hivi karibuni nchini   Thailand.

Monday, August 25, 2014

WAZIRI MKUU AWAKERA ASKARI POLISI JIJIJINI MWANZA, AHANI MSIBA NA KUSHINDWA KUMJULIA HALI ASKARI ALIYEJERUHIWA WAKATI AKIPIMA AJALI ILIYOSABABISHA KIFO CHA MTOTO WA WAZIRI.

  HATUA ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenda kuhani msiba wa mtoto wa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga ‘Mawe Matatu’, bila kufika hospitalini Bugando kumjulia hali askari aliyejeruhiwa vibaya wakati akipima ajali iliyosababisha kifo hicho, imewakera askari polisi wakidai hawathaminiwi.
Pinda ambaye alikuwa mkoani hapa kwa ajili ya kuendesha harambee ya Taasisi ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alifika nyumbani kwa Kitwanga eneo la Misungwi juzi, kuhani msiba wa mtoto huyo, Vedastus Kitwanga, aliyepata ajali mbaya Agosti 19 mwaka huu, eneo la Njia Panda ya barabara ya Tanesco na Bandari wakati akimsaidia mwenzake aliyekuwa amepata ajali awali.
Wengine waliyofika kwa Kitwanga ni Mzee Mkapa na Mama Salma Kikwete, ambapo baadhi ya askari waliliambia gazeti hili kwamba, kitendo hicho cha viongozi kuishia nyumbani kwa kiongozi mwenzao pasipo kwenda Bugando kumjulia hali askari aliyejeruhiwa akitimiza majukumu ya kitaifa ni ubaguzi na kutowathamini.
“Sawa wana utashi wa kwenda kumfariji yeyote, lakini huyu askari mwenzetu WP 4132 Koplo Hamida aliyelazwa Bugando alijeruhiwa wakati akipima ajali iliyosababisha kifo cha mtoto wa Kitwanga. Huyu naye bado alihitaji faraja ya viongozi wetu hao, ila hawakufanya hivyo…
“Pinda alikuwa hapa mjini, ameendesha vikao vya CCM usiku na kutangaza nia ya kugombea urais, halafu kesho yake akapata muda wa kwenda Wilaya nyingine ya Misungwi kwa Kitwanga kuhani msiba wa mtoto wake, lakini Bugando pamekuwa mbali… Labda kwa sababu Hamida si mtoto wa kiongozi,” walidai askari hao walioomba kuhifadhiwa majina yao.
Vedastus Kitwanga na rafiki yake Gasper Mroso, walifariki ajalini kwa kugongwa na gari wakati walipokwenda kumsaidia mwenzao aliyekuwa amepata ajali eneo hilo, ambako wakati WP Hamida akiendelea kupima ajali hiyo, ghafla lilitokea gari lingine na kuwagonga wote.
Inaelezwa kuwa, awali mwenzao huyo alimpigia simu Mroso kumwomba afike eneo
la ajali, ambaye naye alimpigia simu mtoto wa Kitwanga na wakati wakiwa eneo la ajali ndipo likatokea gari lingine likawagonga na kusababisha kifo cha Vedastus pale pale huku Mroso akisagika vibaya miguu yote na kufariki kesho yake akipata matibabu Bugando.
WP Hamida ambaye ni askari wa kituo cha Nyamagana jijini hapa, alijeruhiwa vibaya ambako amelazwa Bugando pamoja na Kombo Mohamed aliyekatika miguu yote.TANZANIA DAIMA

Libya:Uwanja wa ndege wa Tripoli watekwa

Muungano mmoja wa wanamgambo nchini Libya unasema kuwa umeuteka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli baada ya mapigano makali kati yake na kundi pinzani la waasi.
Picha zilizowekwa katika mtandao zimeonyesha wapiganaji hao wakisherehekea juu ya ndege na katika majengo ya uwanja huo.Muungano huo unaoshirikishawanamgambo wa kiislamu pamoja na wanamgambo kutoka mji wa Misrata umesema kuwa uliuteka uwanja huo licha ya mashambulizi ya angani yanayodaiwa kutekelezwa na Misri pamoja na nchi za ufalme wa kiarabu.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli anasema kuwa kuna ripoti za kuendelea kwa vita kati ya makundi pinzani viungani mwa mji huo.Uwanja huo umefungwa kwa takriban mwezi mmoja sasa kufuatia vita kati ya makundi pinzani ya wanamgambo yaliozuka tangu kuondolewa madarakani kwa aliyekuwa rais wa taifa hilo kanali Gaddafi mwaka 2011.

Saturday, August 23, 2014

Airtel Money yazindua rasmi huduma ya kutuma/kupokea pesa moja kwa moja kwenye akaunti ya tigo pesa

Mkurugenzi mtendaji wa Airtel Bwana Sunil Colasa akiongea na waandishi wa habari leo hii (hawapo pichani) akiwatangazia kuanza kutumika rasmi kwa huduma mpya ya kutuma na kupokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine moja kwa moja kwenye akaunti  zao za Airtel money, (interoperability) huduma hii ni ya kwanza Duniani ambapo inaaminika kuwa itasaidia sana wateja wa Airtel Money na Wakala kuokoa muda wa kupata na kutoa huduma kwa haraka Zaidi. 
===========  ==========
  • Wateja Airtel Money sasa wanaweza kutuma na kupokea pesa kwenye akaunti zao za Airtel Money toka Tigo Pesa
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imezindua huduma itakayowawezesha wateja wake wa huduma ya Airtel Money kutuma na kupokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine moja kwa moja kwenye akaunti  zao za Airtel money ,  huduma hii ni ya kwanza Afrika na duniani kwa ujumla na hivyo inaweka historia nchini kuzinduliwa ya kwanza kupitia njia ya  mtandao wa simu.

Huduma hii ya kwanza Duniani na Afrika inayohusisha makampuni ya simu Airtel na Tigo ulitangazwa kuwa itaanza kutumika mwishoni mwa mwezi wa Julai na sasa iko tayari ambapo wateja wa Airtel Money  wataweza kutumia  huduma hii kabambe na yenye utofauti kwa inaaminika kuwa ni  rahisi zaidi, salama na ina unafuu katika kutuma pesa kwa kutoka mteja mmoja kwenda mwingine na kuingia moja kwa moja katika (e-wallet) akaunti yake ya simu/mtandao anaotumia na kuweza kuitoa popote alipo.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi wa Airtel Bwana Sunil Colaso alisema” Tunayofuraha kushirikiana na makampuni mengine ya simu katika kuhakikisha tunaendelea kutoa huduma za kisasa, zenye ubunifu na kwa gharama nafuu. Ushirikiano huu utawawezesha wateja wa Airtel kutuma na kutoa pesa kutoka kwenye mitandao mingine . 
 Sasa wateja wetu watapokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine na kuingia moja kwa moja kwenye (e-wallet) akaunti  zao za Airtel money hivyo kuondoa usumbufu ulikuwepo awali  ambapo mteja anapotumiwa pesa kutoka mtandao mwingine alitakiwa kuzitoa ndani ya siku 7.

Kwa uzinduzi huu  leo tunafanya huduma hii ya kifedha kwa njia ya mtandao kukidhi mahitaji ya wateja. Vile vile mawakala wetu pia wamerahisishiwa utoaji huduma  ambapo sasa hakutakuwa na haja ya wakala kupata udhibitisho wa ujumbe kutoka kwa simu ya mteja kabla ya kufanya malipo.  Tunaamini huduma hii itaongeza usalama wa mawakala na wateja nchini, Pia itamuongezea wakala muda wa kuhudumia wateja wengi Zaidi kwa uhakika, haya ni mapinduzi ya huduma za kifedha ambayo tunaamini ni maendelea makubwa ya maboresho ya huduma hii aliongeza kwa kusema Colaso.

Akiongea kuhusu huduma hiyo mmoja wa wakala ambae alijaribu wa Airtel Money Pasco Woiso alisema “Tunafurahia huduma iliyoanzishwa na Airtel kwa kushirikiana  na mitandao mingine,  leo nimeitumia huduma hii kwa mara ya kwanza lakini nimefurahishwa na ufanisi wake na jinsi wateja wanavyoipokea vizuri nikiwapasha habari kuhusu huduma hiii.  
Kwa sisi wakala awali tulikuwa na tatizo la kupata ujumbe wa malipo, kitambulisho cha malipo na pesa kurudi baada ya muda wa siku saba,  lakini kwa sasa ushirikiano huu umeifanya huduma hii ya pesa kwa mtandao kuwa bora zaidi na kupunguza muda niliokuwa nautumia kumuhudumia mteja moja na hivyo.
Ezekiel Kamwaga
Toleo la 367
20 Aug 2014
Asanterabi Malima
UMEPATA kusikia jina la Dk. Asanterabi Malima?
Jambo moja ambalo wanafunzi waliosoma naye nchini Tanzania hawabishani kuhusu Malima ni ukweli kwamba alikuwa ni mwanafunzi mwenye akili nyingi darasani.
Shafii Dauda ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Azania jijini Dar es Salaam, anamkumbuka Asanterabi kama mwanafunzi mwenye akili aliyefanya vizuri sana katika masomo yake ya kumaliza kidato cha nne.
Shafii, ambaye sasa ni miongoni mwa watangazaji na wachambuzi maarufu wa mchezo wa soka hapa nchini alikuwa kidato cha kwanza wakati Malima alikuwa kidato cha nne.
Akili ile ya Malima imemfikisha nchini Marekani ambako sasa amefanya ugunduzi wa kidude chenye saizi ya pini ndogo (milimita 0.250) kinachoweza kubaini magonjwa ya kuambukiza, kansa na moyo katika hatua ya awali kabisa.
Ugunduzi huu, utakapofika mwisho wake, unaweza kuokoa maisha ya watu wengi duniani. Fikiria tu kwamba unakuwa na kifaa ambacho mojawapo ya magonjwa hayo yakikuanza unaubaini mapema na kwenda kutibiwa.
Mamilioni ya watu wataokolewa maisha yao na kijana huyu wa Kitanzania.
“Siku zote nimekuwa na ndoto za kugundua kitu ambacho kitaweza kuokoa maisha ya watu. Baba yangu alifariki kwa ugonjwa wa moyo ambao ungegundulika mapema kama kungekuwa na kifaa kama hiki.
“Kwa sasa sitaweza kuokoa maisha ya baba yangu lakini ninaweza kuokoa maisha ya wazazi au watoto wa watu wengine kutokana na ugunduzi huu nilioufanya. Nafurahi kwamba ndoto yangu imetimia.
“Kansa, baadhi ya magonjwa ya kuambukizwa na magonjwa ya moyo huwa yanachelewa sana kugundulika. Watu wengi hupoteza maisha, na kwa nchi zilizoendelea hutumia pesa nyingi sana kuwatibu waathirika.
“Kifaa nilichogundua ni kidude cha ukubwa wa pini (0.250mm) kinachoweza kupima na kugundua hayo magonjwa mapema. Ili, yaweze kutibika kirahisi, kuokoa maisha na kupunguza gharama,” anasema Asanterabi katika mazungumzo yake na Raia Mwema yaliyofanyika kwa njia ya mtandao juzi Jumatatu.
Asanterabi ni mtoto wa aliyepata kuwa waziri wa fedha wa Tanzania, Profesa Kighoma Ali Malima, aliyefariki dunia Agosti 6, 1995 jijini London, Uingereza, katika mojawapo ya vifo vya kushtusha katika historia ya Tanzania.
Kifaa alichokigundia kijana huyu wa Kitanzania kinafahamika kwa jina la Biolom na ugunduzi huu aliufanya akishirikiana na wanafunzi wenzake wawili wa Chuo Kikuu cha Northeastern kilichopo Boston; Cihan Yilmaz na Jaydev Upponi.
Pamoja na udogo wake, kipini hicho kina jumla ya maeneo manne –yote yenye kazi maalumu, na ubunifu huo tayari umetambuliwa na Serikali ya Marekani.
Katika mazungumzo yake na vyombo vya habari vya Marekani, Asanterabi alipata kusema kwamba vifaa vingi vya kisasa hubaini magonjwa; kwa mfano kansa, katika wakati ambapo ni vigumu mtu kupata tiba na kupona.
“Kazi yetu hii itakapokamilika, tutaweza kubaini magonjwa haraka zaidi na mapema zaidi na hivyo watu watapata tiba mapema na kuokoa maisha.
“Nchini kwangu (Tanzania), akinamama wengi hufariki dunia kwa sababu ya kuugua ugonjwa wa kansa ya kizazi, kifaa hiki kitaweza kusaidia watu wengi kupona kutoka katika matatizo yao,” alisema.
Kidude hicho ni kidogo sana kwa umbo na namuuliza kama wameamua iwapo mtu anaweza kukinunua na kubaki nacho nyumbani akijitazama mwenyewe au ni lazima aende hospitali.
“Dhamira yetu hapo ni kipimo kitumike mtu akienda hospitali au kliniki (for annual check-up). Lakini japokuwa kinafanya kazi, kupata ruhusa kwa kukiingiza kama pini ni vigumu. Tunafanya vipimo (test) kwa kupima damu iliyotoka kwa mgonjwa,” anasema.
Asanterabi ni zao la mfumo wa masomo wa kawaida uliokuwepo hapa nchini miaka michache iliyopita (kabla ya ujio wa hizi za kata na ‘academy’).
Alisoma katika Shule ya Sekondari ya Tambaza jijini Dar es Salaam kwa mwaka mmoja kabla ya kuhamia Azania.
Miaka 20 iliyopita, hizi zilikuwa ni shule zilizokuwa zikichukua watoto waliofaulu vizuri kimasomo miongoni mwa wanafunzi wa shule za msingi za Mkoa wa Dar es Salaam.
“Tambaza nilisoma mwaka mmoja tu lakini kutokana na fujo zilizokuwapo nikahamishwa na wazazi na ndipo nikaenda Azania nilikosoma mpaka kumaliza kidato cha nne. Nashukuru kwamba nilifaulu vizuri kwa kupata daraja la kwanza. Kimsingi, nilipata alama A katika masomo yangu yote,” anasema.
Pamoja na muda wote alioutumia Marekani na umaarufu ambao ameupata kama mmoja wa vijana wenye bongo zinazochemka nchini humo, Asanterabi bado hajasahau maisha ya hapa nchini na, hususan, maisha ya shule.
Kimsingi, Asanterabi anasikitishwa sana na matokeo mabovu ambayo baadhi ya shule alizosoma katika miaka ya nyuma zimekuwa zikiyapata katika miaka ya karibuni.
“Kwa kweli nakumbuka sana walimu wangu. Pale Tambaza, kwa mfano, namkumbuka sana mwalimu mmoja alikuwa anaitwa Mama Msuya, huyu nadhani ndiye alikuwa mwalimu bora kuliko wote pale. Huyu alikuwa anafundisha Jiografia.
“Katika shule ya Azania, namkumbuka sana Mama Shija ambaye naye alikuwa akitufundisha somo la Kemia. Mzizima namkumbuka sana mwalimu mmoja alikuwa anaitwa Thind - best mathematician ever (mwana hisabati bora kuliko wote niliowahi kufundishwa nao).
“Elimu ni sehemu nyingine ambao inanisisimua mno. Nimefuatilia katika tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ( moe.org.tz ) kuwa mwaka 2011, karibu asilimia 50 ya wanafunzi walipata alama sifuri. Tambaza, Forodhani, Kibasila na Azania zilikuwa na watu wenye akili kuliko wote, pengine Tanzania nzima.
“Niko sasa nafanya kazi na vichwa vya bongo huku Marekani tuone tunaweza kufanya nini kutoa mchango kwa "online video learning" (mafunzo kwa njia ya mtandao maana wengi wetu tulisoma bure tu na huo utakuwa sehemu ya mchango wetu kwa Taifa,” anasema.
Kutokana na ubunifu huo alioufanya na wenzake hao, Malima sasa anatakiwa kuanzisha kampuni ambayo itafanya biashara ya ubunifu huo utakaoleta mapinduzi katika sekta ya afya duniani kote.
Haya ni mabadiliko makubwa katika maisha ya Asanterabi ambaye aliwahi kunukuliwa na vyombo vya habari vya Marekani akisema kwamba siasa iko kwenye damu ya familia yao.
Baba yake alikuwa mwanasiasa na msomi maarufu nchini na kaka wa Asanterabi, Adam, sasa ni Naibu Waziri wa Fedha katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete. Pia ndiye Mbunge wa Jimbo la Mkuranga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Kusema kweli mimi sijawahi kujiona kama mjasiriamali (mfanyabiashara). Watu wengi walijua kwamba nitakapokuwa mkubwa nitafuata tu nyayo za wazee wangu. Lakini leo niko hapa.
“Kwenye maisha yangu, sikutaraji kwamba ipo siku nitakuja kufanya ubunifu kama huu. Baada ya kufika hapa nilipofika, sasa naamini kwamba naweza kupiga hatua zaidi,” anasema.
Ingawa fedha si msukumo mkubwa katika maisha ya Asanterabi, ugunduzi huu unaweza kumfanya kuwa mmoja wa Watanzania matajiri endapo kidude hiki kitaanza kuuzwa.
Hesabu zake ziko hivi.
“Tunafikiri kitakapokuwa tayari, kidude kimoja kinaweza kuuzwa kwa wastani wa dola moja hivi ya Marekani (Shilingi 1650) kama tukiweza kufanya uzalishaji mkubwa.
“Gharama ya kupimwa inaweza kugharimu kiasi cha kati ya dola 10-15. Mahospitali huwa wanachaji hela nyingi mno kama daktari ndio atafanya vipimo na maamuzi. Ila kama ni nesi gharama si kubwa,” anasema.
Katika dunia yenye watu zaidi ya bilioni sita, uwezekano wa kuuza pini hizo milioni mia moja kwa mwaka ni mkubwa na kwa kiasi hicho pekee, mauzo ya zaidi ya dola milioni 100 kwa mwaka (zaidi ya shilingi bilioni 165) yanawezekana.
Asanterabi na wenzake watakuwa na mgawo wao hapo na ifahamike kwa sababu ya sheria kali za hatimiliki nchini Marekani, hizi ni fedha ambazo familia ya wagunduzi watakula hadi kwa wajukuu, vitukuu na kuendelea.
Safari ya Asanterabi kutoka Tanzania kwenda Marekani haikuwa rahisa namna hiyo. Ikumbukwe kwamba alifiwa na baba yake wakati ndiyo kwanza akiwa na umri wa miaka 15 tu.
Ni msiba ambao nusura ubadili kabisa maisha ya kijana huyu ambaye baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma naye wanamtambua kwa jina la “Mzaramo wa Chole.”
Chole ni miongoni mwa mitaa maarufu ya eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam ambako Asanterabi alikulia. Pengine, jina hilo linatokana na ukweli kwamba kuna watu wachache wa kabila la Wazaramo analotoka Malima wanaoishi huko.
Majina ya namna hii hayakuwa na maana ya ubaguzi wa kikabila lakini ni sehemu ya utani wa kikabila uliokuwa Tanzania wakati huu.
Utafiti na ubunifu huu wa Asanterabi si habari kubwa hapa Tanzania pekee kwani inaonekana kwamba hata Marekani nako ameanza kutambulika.
Juni mwaka huu, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Wiki ya Afrika katika Jimbo la Massachussets uliko mji wa Boston, Gavana wa Jimbo hilo, Deval Patrick, alimpa Asanterabi tuzo maalumu ya Ujasiriamali akimpongeza kwa ubunifu wake huo utakaosababisha nafuu kwa maisha ya wanadamu na pia ukuaji wa uchumi wa eneo hilo.
“Si kwamba ugunduzi huu utabadili maisha ya wengi na uchumi kwa wakazi wa Marekani pekee, lakini ugunduzi huu utasaidia sana kuokoa maisha ya mamilioni ya wananchi katika nchi anakotoka Malima ya Tanzania,” alisema Gavana huyo.
Miaka michache iliyopita, Asanterabi alikuwa akijipanga kuwa mmoja wa waajiriwa katika mojawapo ya kampuni kubwa duniani ya Toshiba, lakini sasa ugunduzi huu umemfanya kujiandaa kuwa mmoja wa viongozi wa kampuni muhimu hapa duniani.
Pamoja na umbali mkubwa uliopo sasa, baadhi ya watu wanaomfahamu Asanterabi wanamkumbuka kama kijana mpole ambaye hakuharibiwa na ukubwa wa jina la baba yake.
“Mzaramo wa Chole alikuwa mpole sana kipindi kile anasoma Azania na kwa kweli hakuwa na mambo mengi kama walivyo watoto wengi wa wakubwa,” anasema Mintanga Malulu aliyesoma katika shule hiyo wakati mmoja na Asanterabi.
Jambo zuri kuhusu Asanterabi ni kwamba ni mzalendo na anayependa nchi yake. Katika mazungumzo yake na Raia Mwema, alisema kwamba kwa namna yoyote ile ugunduzi wake huo utaifaidisha Tanzania.
Tayari Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (Costech) imetangaza kuvutiwa na mafanikio ya Asanterabi katika Nyanja hiyo ya sayansi.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Dk. Flora Tibazarwa, inasema ingawa utafiti huo bado haujafikia katika hatua ya mwisho, matumaini ni makubwa.
“Tuna taarifa kuhusu ugunduzi wa Dk. Malima lakini hatuwezi kusema chochote kwa sasa kwa vile bado uko katika hatua za awali na haujapita katika vipimo vyote. Jambo zuri ni kwamba dalili za kufanikiwa ni kubwa,” ilisema taarifa hiyo.
Ni safari ndefu, ndefu sana kutoka Tanzania hadi Marekani. Lakini, kama mwisho wake ni kama ule wa Asanterabi, safari inakuwa njema.
Wakati tukiagana baada ya kumaliza mazungumzo yetu, bado alionyesha kusikitishwa na matokeo katika shule za sekondari maarufu; Hivi, kuna nini kinatokea huko kwa Azania na Tambaza?
Sikuwa na majibu. Labda nitapata kama nitafanya utafiti. Labda, itabidi Asanterabi agundue kidude kingine kitakachotoa majibu kuhusu kushuka kwa elimu hapa nchini.
Swali moja kubwa ambalo nimejiuliza baada ya mazungumzo yangu na Asanterabi ni moja tu; Hivi kweli Taifa hili litakuja kutoa akina Asanterabi wengine katika miaka 20 ijayo  katika mfumo wetu wa elimu tulionao sasa?
- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/asanterabi-malima-mtanzania-atakayeokoa-dunia#sthash.srse7bfH.VDkOp2kH.dpuf

WAZIRI MKUU PINDA AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA JAJI MAKAME

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole Jaji Leila Makame Mgonya mmoja wa wana familia, wa Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Marehemu Jaji Lewis Makame baada ya kuzungumza kwa niaba ya serikali na kutoa heshima za mwisho kwa marehemu huyo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam August 22, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimian na Mawaziri Wakuu, Wastaafu, Frederick Sumaye na Jaji Joseph Warioba (wapili kulia) kabla ya kuzungumza kwa niaba ya serikali na kutoa heshima za mwisho kwa Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, marehemu Jaji Lewis Makame kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam August 22, 2014. Kulia nI jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman. 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na jaji Mkuu Mohamed Chande Othman (kulia) na Mawaziri Wakuu Wastaafu, Joseph Warioba (wapili kulia) na Frederick Sumaye kabla ya kutoa salamu za Serikali na heshima za mwisho kwa Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, marehemu Jaji Lewis Makame kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam August 22, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitoa heshima za mwisho kwa Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Marehemu Jaji Lewis Makame baada ya kuzungumza kwa niaba ya serikali kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam August 22, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wednesday, August 20, 2014

TANZANIA TO BENEFIT FROM ABE INITIATIVES

 Deputy Permanent Secretary President's Office-Public Service Management Mr.HAB Mkwizu (left) present a gift to outgoing JICA Senior Representative Mr. Hajime Iwama during a farewell ceremony held at the President's Office-Public Service Management yesterday.
 Deputy Permanent Secretary President's Office-Public Service Management Mr.HAB Mkwizu (left) speaking at a farewell ceremony of departing JICA Senior Representative Mr.Hajime Iwama (second left) at the President's Office - Public Service Management yesterday.
Deputy Permanent Secretary President's Office-Public Service Management Mr.HAB Mkwizu (second left) in a group photo with JICA staffs, and President's office officials after a farewell of departing JICA Senior Representative Mr.Hajime Iwama (right,first line) held at the President's Office-Public Service Management yesterday.

TANZANIA TO BENEFIT FROM ABE INITIATIVES

By Happiness Shayo.

The Government of United Republic of Tanzania is among four African countries that benefits from Master’s Degree and Internship Program of the African Business Education Initiative for Youth (ABE Initiative) initiated by Japanese Government through Japanese Prime Minister Abe.

Speaking yesterday during a farewell ceremony at the President’s Office, Public Service Management the departing JICA Senior Representative Mr. Hajime Iwama said that the program supports youth who have potential to contribute to their countries.“This program will support young men and women from Private and Government Sectors to study Master Courses in Japanese Universities as international students and experience internships at Japanese enterprises.”

He said the aim of the program was to develop effective skills and knowledge so that they can contribute to the development of their societies. He listed other countries which benefits from the program as Republic of Kenya, Republic of Mozambique and Republic of South Africa.

Mr. Iwama explains that the implementation of the program started this year whereby 33 Tanzanians have been selected to attend Master’s Degree Program in Japan.Meanwhile, Deputy Permanent Secretary; President’s Office Public Service Management Mr.HAB Mkwizu said that JICA has been very instrumental in supporting Tanzania’s development through soliciting and allocating volunteers and experts to serve the needs of the people in different parts of the country.

He mentioned among the sectors supported by government of Japan through JICA as health, education and infrastructure development among others.Mr. Mkwizu assured JICA Reprentatives that Tanzania will continue to sustain the programmes and projects initiated by JICA in order to deliver desired benefits to the intended communities.

Sunday, August 17, 2014

JAJI WEREMA APINGANA NA IKULU ,ASEMA BILA UKAWA HAKUNA KATIBA

IMG_0173Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema akitoa ufafanuzi wa masuala Kisheria kwa waandishi wa habari kuhusu mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
IMG_0197Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema akiwaonesha waandishi wa habari Rasimu ya katiba wakati akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kisheria katika mchakato wa Katiba wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam 
IMG_0199
IMG_0206 Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Na Rose Masaka-MAELEZO
Viongozi wa vyama vya siasa waliopo nje ya Bunge Maalumu la Katiba wameaswa kurejea bungeni ili kufanya maridhiano ndani ya bunge hilo.
Kauli hiyo imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam.
Jaji Werema amesema kuwa wajumbe walio nje ya Bunge Maalum hawana budi kurejea bungeni na kuacha kumshinikiza Rais kulivunja bunge hilo kwani hana mamlaka ya kulivunja kulingana na sheria inayoliongoza bunge hilo.
“Sheria inasema kuwa baada ya bunge hilo linaweza kuvujwa baada ya katiba kupatikana, kinyume na hapo bunge husitishwa kufikia maridhiano na kufikia mwafaka kwa kufuata misingi ya demokrasia.” alisema Jaji Werema.
Pia Jaji Werema alisema kuwa wajumbe walio nje ya bunge hilo hawana budi kurudi ili kuendelea kujadili vipengele vingine vya rasimu ili kuweza kupata katiba iliyo bora kwa nchi na watu wake.
Aidha, Jaji Werema aliviasa vyombo habari kutumia nafasi yao ya kuwa mhimili muhimu katika uongozaji wa nchi kutokuwa na upendeleo katika utoaji wa taarifa na kuacha kuongozwa na mawazo ya wachache ili kuweza kusaidia nchi kupata Katiba Mpya kwa manufaa na maendeleo ya nchi.